Khalil

Mtu mwenye ukatili hata tungeweza kumwita gaidi, alibadilika kutoka kuwa mwuaji "Sauli" na kuwa mtu aliyeweza kusamehe wengine "Paulo" baada ya kutembelewa na Isa al Masih kwa ndoto iliyomwingia moyoni mwake. Mtu huyu aliyekuwa amewachukia Wakristo hata na Wayahudi, alipanga mpango wa kuidhalilisha Injili. Hatimaye badala yake yeye mwenyewe alibadilishwa kabisa wakati ule Isa al Masih alipomtokea na kubadilisha moyo wake.